top of page

UKAMUAJI WA MAZIWA YAKO KWA MKONO

Ukamuaji kwa mkono ni ujuzi kila mama anayenyonyesha anaweza kujifunza. Mama wengi hawana pampu ya matiti. Wao hukamua na mkono ili kuachiaa maziwa watoto wao. Matiti yako yanajua joto la ngozi-kwa-ngozi, kwa hivyo mikono yako kwenye ngozi yako si ngeni na inaweza kusaidia kutoa maziwa zaidi kutoka kwenye matiti yako. Hauitaji chochote isipokuwa mikono yako!

 

SABABU ZA KUKAMUA KWA MKONO

Maziwa yako ndio chakula bora kwa mtoto wako. Unaweza kuhitaji kukamua maziwa yako:

  • ikiwa mtoto amezaliwa mapema sana na bado hawezi kunyonya.

  • ikiwa mtoto ni mgonjwa sana kuweza kunyonya vizuri.

  • ikiwa unasikia matititi yako yakiwa yamejaa sana baada ya kujifungua na unahitaji kupunguza shinikizo.

  • ikiwa unahitaji kutengenezea mtoto wako maziwa Zaidi.

  • ikiwa uko mbali na mtoto wako na unahitaji kumuachia maziwa.

Wamama kawaida hupata maziwa zaidi wakati wanapotumia mikono yao, badala ya pampu tu.

 

NJIA YA RAMANI YA KUKAMUA KWA MKONO

Hii hapa ni njia rahisi ya kukamua maziwa yako:

  • Mwanzoni, kutoa maziwa nje ni sawa. Weka bakuli pana kwenye paja lako kukamata maziwa, ukisoga kwenye bakuli ndogo, halafu kikombe ukiona ni rahisi. Akina mama wengine huwa wazuri sana baada ya muda kwamba wanaweza kuweka kikombe mbele ya kila titi na kufanya vyote mara moja. Weka kitambaa kwa urahisi ikiwa utanyunyizia kila mahali.

  • Kwa mikono safi, anza kwa kupatia matiti yako mtetemsho na muamsho kiasi na kwa upole uvute chuchu.

  • Weka kidole gumba na kidole cha juu karibu sentimita 1 nyuma ya chuchu yako. Hii inaweza kuwa au kutokuwa kwenye areola yako (ngozi nyeusi karibu na chuchu). Weka vidole kwenye umbo la C na usinyweshe kifua chako (ngozi kati ya kidole gumba na kidole cha mbele haipaswi kuwa kwenye kifua; unapaswa kuona nafasi wazi).

  • Rudisha matiti yako kwenye ukuta wa kifua.

  • Tembeza vidole vyako kana kwamba unachukua alama za vidole.

  • Rudia hii kwa utungo.

  • Utajua una vidole vyako mahali inayotakiwa ikiwa utaanza kuona matone ya maziwa, kisha mnyunyizo na kisha maziwa ikipita vizuri.

  • Zungusha karibu na matiti ili ufanye kazi kwenye mifereji karibu na matiti na sio upande mmoja tu.

  • Usitandaze vidole vyako, usibane, usiteleze na usivute chuchu yako kwani hizi zote zinaweza kusababisha maumivu na uharibifu.

© 2025 by La Leche League South Africa. Read our Privacy Policy here. Read our PAIA Manual here.

  • Facebook Social Icon
MySchool button.png

All images and other materials posted on this site are subject to copyrights owned by La Leche League South Africa or other individuals.  Any reproduction, retransmission, distribution or republication of all or part of any images, and other materials found on this site is expressly prohibited, unless La Leche League South Africa or the copyright owner of the material has expressly granted its prior written consent.  All other rights reserved.  

bottom of page